sw.news
103

Francis Amwaibisha Kadinali Sarah Hadharani

Mnamo tarehe 22 mwezi Oktoba Papa Francis alitoa barua ya wazi aliyomwandikia Kadinali Sarah ambapo anakosoa kauli aliyoitoa Sarah hivi maajuzi kuwa bado shirika lake ndilo lenye mamlaka juu ya tafsiri za kiliturujia.

Francis alisisitiza kuwa nakala ya Magnum Principium bila shaka huyapatia mabaraza ya Maaskofu mamlaka juu ya tafsiri za kiliturujia. Desturi za hapo awali hazitumiki tena. Francis alimwamuru Sarah kutuma marekebisho ya hadhara kwa mitandao ambayo ilitangaza kuhusu kauli yake hiyo, na kwa mabaraza yote ya maaskofu.

Picha: Robert Sarah, © Antoine Mekary, Aleteia, CC BY-NC-ND, #newsTaocqpvlhk