sw.news
39

Kadinali Zen, Makubaliano Ya Vatikani Na China Ni "Bandia"

Makubaliano kati ya Vatikani na China huenda yakalitia Kanisa Katoliki mchini humo katika "kizimba", Kadinali Joseph Zen, mwenye umri wa miaka 86, wa Hong Kong alisema.

Akizungumza na Associated Press (Februari 9), Zen alieleza kuwa Serikali ya China inataka Kanisa Katoliki lisalimu amri ili wapate udhabiti kamili.

Kuhusu mipango ambayo huenda ikampa Papa nguvu katika uteuzi wa Maaskofu wa siku za usoni, Zen alisema, "Hilo linasikika kuwa jambo zuri, ila ni la bandia". Kulingana na Zen Papa hawezi kuyatumia mamlaka yake hayo mara nyingi. Zen angependelea utaratibu ambapo Papa ndiye mwenye kuwateua maaskofu huku China ikiwa na mamlaka kiasi.

Picha: Joseph Zen, © Mazur, catholicnews.org.uk, CC BY-ND, #newsKczsdbanwn