sw.news
75

Habari Za Kipekee Na Za Kuvunja Moyo Zilizotangazwa Na AP Zinamshambulia Francis

Habari za kipekee zilizotangazwa na kituo cha AP (Februari 6) zimegundua kuwa Papa Francis alipokea mnamo mwaka wa 2015 barua ya kurasa nane kutoka kwa Juan Carlos Cruz ambaye sasa huishi mjini Philadelphia, na mwadhiriwa asemekanaye kuwa alidhulumiwa na Padre wa Chile Fernando Karadima. Barua hiyo ilieleza kwa kina jinsi Karadima alivyomdhulumu Cruz kingono na jinsi ambavyo wachungaji wengine wa Chile, akiwemo Askofu Juan Barros wa Osorno, Chile, walivyosemekana kulipuuza jambo hili.

Maduai ya dhulma za kingono zake Karadima hazijapingwa. Kilichopingwa ni madai kuwa Askofu Barros ambaye kwa wakati huo alikuwa rafikiye Karadima, alijua kuwahusu.

Hapo awali, Francis alimtetea Barros vikali na kuyaita madai dhidi yake "uchochezi”. Habari hizo za kipekee za AP hazitoi maarifa mapya kumhusu Barros ila zimevutiwa sana na lengo la kuibua hisia tofauti dhidi ya Francis.

Picha: © Marko Vombergar, Aleteia CC BY-SA, #newsDvpqyzifml