sw.news
37

Habari Za Mashtaka Ya Siri ya Pell Zimeibuka

Katika majuma manne ya kusikizwa kwa mashtaka dhidi ya Kadinali George Pell mashtaka hayo ya uongo pamoja na ushahidi unaosemekana yamefichwa kama siri.

Lakini kulingana na TheAge.com (Machi 30) habari kuhusiana na mashtaka hayo ya uongo zimeibuka.

.• Pell ameshtakiwa kwa madai ya kuwadhulumu kingono wanakwaya wawili katika Kanisa kuu la Mtakatifu Patrick la Melbourne mwishoni mwa miaka ya 1990 alipokuwa Askofu mkuu wa Melbourne ingawaje wakati wa matukio haya hakuwa peke yake na wanakwaya wengine walikana kuona jambo lolote la kushukiwa.

• Ameshtakiwa kwa kutenda makosa katika kidimbwi cha Ballarat lakini wafanyikazi walikana kuwahi kuona jambo lolote la kudhaniwa viovu.

•Ameshtakiwa kwa kufanya makosa katika ukumbi wa sinema wakati wa maonyesho ya "Close Encounter of the Third Kind" mwishani mwa miaka ya 1970. Lakini meneja wa ukumbi huo alisema kwamba hakumbuki akiwona Pell kwenye ukumbi huo.

Wakati wa kusikilizwa kwa kesi hiyo, Kadinali Pell alidumisha tabia yenye upole mwingi.

#newsBbgsvkdron