sw.news
73

Kano La Vatikani Lina Uaminifu Mdogo Sana

Msemaji wa Vatikani Greg Burke alikana kuwa Vatikani ilikinga kabisa mtandao wa correctiofilialis.org licha ya kiwa mtandao huo haungefikiwa kutoka kwa tarakilishi za Vatikani.

Kulingana na Il Giornale Burke alisema kuwa mtandao wa correctiofilialis.org ulizuiliwa na programu atomatiki ambazo, pamoja na vitu vingine, huingilia maombi ya kupata habari za kibinafsi, kama vile ukurasa wa kujisajili kwenye mtandao huo wa correctiofilialis.org.

Maelezo ya Burke yana uaminifu mchache sana. Ukurasa huo wa kujisajili unaosemekana ninwa aina ya "overlay" ambao hutumika na JavaScript. Lakini programu anazosema, huwa hazitumii JavaScript na hivyo basi haziwezi kugundua ukurasa huu ukiitisha habari za kibinafsi.

Maelezo ya Padre mwenye taabu, kinara wa Mawasiliano, Dario Viganò, yalikuwa hayana uaminifu wowote. Alisema kuwa programu hizo za Vatikani huwa hazikubalishi mitandao ya aina ya "parked domain site" , hii ni kumaanisha, mitandao isiyo na habari halisi ila tu viungo. Bila shaka huu sio ukweli kwani kinyume na walivyosema mtandao wa correctiofilialis.org umejawa na habari nyingi.

Picha: Greg Burke, © Mika58, wikicommons, CC BY-SA, #newsPprfhgbjhq