sw.news
64

Ujerumani: Mwislamu Amwita Kasisi "Nguruwe" Hadharani - Hakuna Kilicho Tendeka

Mwislamu alimtukana kasisi wa Werl, katika Dayosisi ya Paderborn, nchini Ujerumani, alipokuwa akiondoka kweye duka, kulingana na taarifa iliyochapishwa kwenye nakala za paroko hiyo.

Kasisi huyo, aliyekuwa kavalia mavazi ya uchungaji, alikuwa akisubiri kwenye foleni ya kufanya malipo. Mwanamke mwislamu aliyekuwa na mtandio alikuwa mbele yake. Bwanake alimwendea kasisi huyo huku akimkemea kwa lugha ya kigeni. Kiimbo chake kiliashiria kuwa alikuwa akimtukana kasisi huyo

Kasisi huyo alikipuuza kitendo hicho. Mwanaume huyo alipoanza kukiskuma kikapu chake, Kasisi huyo alimwambia kwa upole kuwa "unaweza kuniongelesha kwa Kijerumani kwani naielewa lugha hiyo". Mwanaume huyo alimjibu kwa Kijerumani, "Wewe Kafiri!", "Wewe nguruwe!".

Bila kusema lolote, Kasisi huyo alichukuwa simu ya rununu na kuwapigia polisi. Aliambiwa kuwa polisi "hawakuwa na maarifa" ya kukabiliana na hali kama ile. Wengi wa waliosaidia katika kutatua suala hilo walikuwa na Woga.

Picha: © Garrett LeSage, CC BY-NC, #newsAxyylxugla